Friday, May 4, 2012

Uongezekaji wa uzito kwa mama Mjamzito


Wanawake wengi huwa wanaogopa kuongezeka uzito sana wakati wa ujauzito kwa sababu ya kupoteza mvuto wao baada ya kuzaa. Kitu ambacho unabidi ukumbuke ni kwamba ukila chakula chenye afya kwa mama mjamzito basi uzito wote utakaoupata kwa wakati huu ni ule ambao mwili wako unauhitaji.

Katika kipindi hichi mwili hufanya kazi kubwa sana katika kutengeneza viungo vya mtoto na pia katika kuujenga mwili wa mama ili uweze kusupport na kumtunza mtoto kwa kipindi kizima cha ujauzito.

Wamama wengi husikia njaa sana wanapokuwa wajawazito na huwa na hamu kubwa ya kula hii ni njia ya mwili kumkumbusha mama kutosheleza mwili kwa ajili ya kipindi hiki maalum. Pamoja na hayo usichukulie hii kama sababu ya kula chakula chochote kile. Mama anabidi apate virutubisho vizuri vinavyotakiwa kwa afya yake na mtoto.

Kula chakula ambacho kina diet na balanced especially kwamama mjamzito ambacho kina protein ya hali ya juu. Usile vyakula vyenye mafuta mengi, sukari au vyakula vya junk food.

Kitu muhimu kwa mama mjamzito ni kuhakikisha hali vyakula vilivyotengenezwa viwandani yaani processed food na junk food, pia vyakula ambavyo haviko natural kwani hivi vinasababisha unene bila kuupa mwili au mtoto virutubisho vya kutosha.

Hivyo mama anahitaji ahakikishe kuwa anakula vyakula natural vilivopikwa nyumbani vyenye protein ya kutosha. Kumbuka ubongo wa mtoto na wa mama umetengenezwa na 75% ya mafuta ya cholesterol. Na ni muhimu sana mama kutosheleza mahitaji yake ya cholesterol kutoka kwenye vyakula vyenye protein ya juu kama vile maziwa. Ndio maana maziwa ni muhimu sana kwa mtoto anayekua ili kuutengeneza ubongo wake.

Je, unapopima uzito huo uzito unaongezeka mwilini huenda wapi? Kumbuka sio uzito wote unaoongezeka wakati wa ujauzito ni uzito wa kunenepa bali:

  • 7.5 – 8 pound ni uzito wa mtoto
  • 2 pound ni za amniotic fluid( yale maji ambayo yanamlinda mtoto ndani ya uzazi)
  • 1.5 – 2pound ni placenta( mfuko wa uzazi)
  • 1.5 -2pound zitaenda kwenda kwenye maziwa kutayarisha utengenezaji wa chakula cha mtoto atakapozaliwa
  • 3lb ni damu ambayo itaongezeka mwilini kuhakikisha unadamu ya kutosha
  • 2 – 2lb misuli ya uzazi
  • 4 pound maji
  • 8 pound ni mafuta ya akiba kutosheleza mwili na kukupa nguvu ya kila siku.

Kwa mara nyingi mama mjauzito anashauriwa aongeze uzito kati ya 25 pound mpaka 35 pounds lakini usifuatishe sana hizi namba kwani kila mtu ni tofauti. Ili mradi unakula chakula bora kwa mama mjamzito basi usiwe na wasiwasi wa kuongezeka kwani mwili wako unajua ni kiasi gani unahitaji kwa ajili yako na mtoto.

Pia ukumbuke kuwa kutokuwa na uzito wa kutosha utasababisha mtoto kuzaliwa na uzito mdogo ambayo ni chini ya 5 pounds hii inaweza kusabibisha mtoto kuzaliwa na magonjwa au kushindwa kukua vizuri au kuzaliwa njiti.

Pia ukiongezeka uzito kupita kiasi kutafanya mtoto awe na uzito mkubwa kupita kiasi kitu ambacho kitasababisha kuongezeka muda wa labour, matatizo ya kuzaa, kuzaa kwa operesheni au c-section.

Hivyo ni muhimu sana mama kubalance na kuongezeka kwa uzito unaotakiwa kwa afya yake na mtoto.
Pamoja na kula chakula bora kwa mama kumbuka kupata mazoezi maalum ya mama mjamzito ya kutosha kila siku. Hii itasaidia mwili wako kutumia virutubisho vya chakula vizuri na itasaidia pia pale utakapozaa mwili kurudi kiurahisi zaidi.

Kuhusiana na upunguaji wa uzito wa uzazi, ni kweli kila kukicha tunasikia story za watu maarufu au macelebrity ambao wamepungua sana pale wanapotoka kuzaa na hivyo wanawake wengi huwa na dhamira ya kupungua tu pale watakapozaa. Ila ni vizuri kukumbuka kuwa ulitumia miezi tisa kuongezeka mwili wako ili kujitosheleza wewe na mtoto hivyo vile vile jipe japo miezi tisa ili upungue.

Sasa nitashare personal story yangu, naweza kusema baada ya kuzaa mtoto wangu uzito ule wa placenta, maji, mtoto ulisababisha uzito wangu upungue kwa kiasi kikubwa na mazoezi niliyokuwa nikiyafanya wakati wa ujauzito na vile vile kunyonyesha kulinisaidia sana.

Nilirudi katika uzito wa zamani hadi nikapatiliza, mwenyewe nilifurahi sana. Lakini nilikuwa naambiwa labda sili vya kutosha. Lakini hiyo haikuwa sababu kwasababu nilikuwa nakula sana na appetite yangu ilikuwa kubwa mno, ni mwili tu ulikuwa unajaribu kujirekebisha baada ya kumaliza kazi moja na kujitayarisha kwenda katika kazi ya pili ya kumnyonyesha mtoto aliyezaliwa. 

Pia kumbuka katika muda huu mama anakuwa hapati usingizi wa kutosha kwasababu ya kuamka kumhudumia mtoto na wengine huwa hawana wasaidizi nyumbani hivyo wanabidi pia waendelee kufanya kazi muhimu za ndani. Hivyo mwili pia bado unajaribu kujijenga kwa sababu ya uchovu na kazi ya kuzaa.

Ni katika kipindi hiki mama anaweza kudhani kuwa ameweza kumaintain kurudi katika uzito wake wa zamani.

Lakini kitu kilichotokea baada ya hapo ni kuwa kwa vile nilikuwa nanyonyesha appetite yangu iliongezeka kwa kiasi kikubwa ili kutosheleza kutengeneza chakula cha mtoto na pia kuuguza mwili kutokana na kazi iliyoifanya ya kuzaa. 

Basi mtoto alipoacha kunyonya baada ya kama mwaka mmoja na nusu hivi mimi nilikuwa nishazoea kula kiasi kikubwa kupita zamani. Sasa mtoto kaacha kunyonya na mimi nakula kama vile bado natengeneza chakula cha mtoto. Basi hapo katika hicho kipindi ndio nikaanza kunenepa, hadi mwili ulipobaini kuwa hauhitaji tena kutengeneza chakula cha mtoto na matumizi kupungua ndio appetite kupungua na ndio mwili ukaanza kurudia tena hali ya awali. 
Katika muda huu mama anakuwa tayari anaweza kurudi katika diet yake ya kawaida na kufanya mazoezi ili kufikia lengo lake la kupungua kwa usalama zaidi.

Je wewe kama umeshazaa unaexpereince gani katika uongezekaji wa uzito? unaweza kutuma comment yako hapo chini au kutuma email kama unataka kuuliza swali mwanamkeuzazi@gmail.com

No comments:

Post a Comment