Sunday, February 19, 2012

Afya Yako kabla ya Ujauzito

 

Mayai ya mwanamke ni mojawapo ya viungo ambavyo vimeshatengenezwa kabla hata mwanamke hajazaliwa, yaani tangia akiwa fetus ndani ya tumbo la mama yake. 

Haya mayai yanakuwa tayari pale msichana anapopata menstruation yake ya kwanza average ya miaka 12 hadi 14. Kuanzia hapo hadi pale atakapofikia menopause/kikomo cha menstruation kwa mwanamke (average miaka 51) mayai yake na fertility yake hupungua anavyozidi kuzeeka. Yaani katika ujana wake, teenage na 20s ni muda ambao ni rahisi zaidi kutunga mimba. Na kuanzia miaka 30 had 51 uwezo huu unapungua kwa kiasi kikubwa mpaka unapoisha kabisaa.

Wakati kwa wanaume wao sperm cell zinaanza kutengenezwa pale wanapo balehe(puberty age) mpaka siku atakayo kufa. Hii inamaanisha kama mwanaume akiwa katika hali nzuri ya kiafya anaweza kumpa mimba mwanamke hadi afikapo uzeeni iwapo mwanamke bado hajafikia menopoase na ni fertile. 

Sasa tuangalie ni vitu gani vinaweza kuaffect kwa kiasi kikubwa utungaji wa mimba(fertility).
Wanaume na wanawake wanaweza kuwa affected na vitu kama kemikali katika mazingira ya kila siku, diet au lishe na hata matukio mbali mbali katika maisha kama stress.

Hii inaweza hata kuaffect quality ya mayai au sperm ambayo pia inaweza kumuaffect mtoto.

Basi kama wewe na mwenzi wako mnajitayarisha kupata mimba mnapaswa miezi kadhaa kabla muache vitu vifuatavyo:
  • Kunywa dawa mara kwa mara kama si lazima (zikiwemo aspirin na antibiotics)
  • Utumiaji wa hali ya juu wa vinywaji vikali, pombe na wine
  • Caffeine (kahawa, black tea, cola, chocolate)
  • Utumiaji wa sigara
  • Hakikisha wote mnakula vyakula ambavyo ni balanced diet.(nitafafanua zaidi maana ya balanced diet katika nakala zijazo)
  • Radiation inayoambatana na x-ray na teknologia zingine
  • Rangi na dawa za kubadilisha nywele
(Hii list ni baadhi tu ya vitu, kwa wale ambao wangependa list kamili basi wanaweza wakaomba katika comment au kupitia e-mail yetu.)

Hii haimainisha ya kuwa usipoachana na hivi vitu huwezi kupata mimba la hasha. Bali kama wewe tayari una matatizo au unataka chance ya kupata mimba kuongezeka haya mambo yanaweza kusaidia. Na kama ungependa kuwa na mimba yenye afya njema(healthy pregnancy) na mtoto mwenye afya njema basi unabidi uzingatie hivi vitu (hasa hasa kama ungependa kuhakikisha ukuaji mzuri wa ubongo wa mtoto yaani brain development). 
Hii pia itasaidia kwa kiasi kikubwa kupunguza matatizo yanayoweza kutokea wakati wa uzazi.

Kama wewe unamatatizo ya fertility au kupata mimba basi hapo mbeleni tutaongelea vyanzo na njia mbalimbali zinazoweza kusaidia upatikanaji wa mimba.

No comments:

Post a Comment